Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Kitabu kuhusu malengo ya milenia chapata tuzo

Kitabu kuhusu malengo ya milenia chapata tuzo

 

Jumla ya mashirika sita ya Umoja wa Mataifa yametunukiwa tuzo la mwaka huu la amani na michezo kutokana na mradi wao wa kitabu cha vichekesho chenye kichwa ‘Funga mabao – Kuungana katika kutimiza malengo ya milenia’. Tuzo hiyo ilitolewa mjini Monaco kwenye kongamano la kimataifa kuhusu amani na michezo mbele ya watu 500 mashuhuri kwenye nyanja za siasa, michezo , sekta za kibinafsi na mashirika ya umma. Mradi huo ulitunukiwa kutokana na jitihada zake za kuhakikisha kuwepo kwa amani na uwiano wa kijamii mwaka huu wa 2011. Flora Nducha anaripoti

(RIPOTI YA FLORA NDUCHA)