Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Pillay ataka jamii ya kimataifa kuchukua hatua nchini Syria

Pillay ataka jamii ya kimataifa kuchukua hatua nchini Syria

Mkuu wa haki za binadamu kwenye Umoja wa Mataifa Navi Pillay ameitaka jamii ya kimataifa kuchukua hatua za haraka ili kuwalinda raia nchini Syria ambapo idadi ya waliouawa sasa imefikia watu 3000 wakiwemo watoto 180.

Pillay amesema kuwa tangu kuanza kwa ghasia nchini Syria serikali imekuwa ikitumia nguvu kupita kiasi wakati kuvunja maandamano ya amani. Matumizi ya risasi na mashambulizi ya mabomu kwa makaazi ni kati ya mbinu ambazo zimekuwa zikitumika kwenye miji nchi Syria. Pillay pia amesema kuwa maelfu ya watu wengine wamekamatwa , kufungwa huku wengine wakitoweka na kuteswa. Rupert Colville ni msemaji wa ofisi ya haki za binadamu.

(SAUTI YA RUPERT COLVILLE)