Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Kikao kuhusu Somalia chakamilika mjini Copenhagen

Kikao kuhusu Somalia chakamilika mjini Copenhagen

Kikao cha 20 cha kimataifa cha kundi la Somalia, kimekamilisha mkutano wa siku mbili mjini Copenhagen, nchini Denmark. Mkutano huu umezungumzia mipango wa kumaliza kipindi cha mpito cha serikali ya mpito ya Somalia ifikapo Agosti 12. Mjumbe maalum wa UM nchini Somalia balozi Augustine Mahiga, alihudhuria kikao hicho wakiwemo wawakilishi kutoka Marekani na Norway. Balozi Mahiga aliongea kuhusu suala hili na redio ya UM.

(SAUTI YA BALOZI MAHIGA)