Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UM washtushwa juu ya mauwaji ya kutisha yaliyofanyika Libya

UM washtushwa juu ya mauwaji ya kutisha yaliyofanyika Libya

Umoja wa Mataifa umesemwa kuwa umeshtushwa juu ya ripoti zinazosema kuwepo kwa mauwaji ya mamia ya watu pamoja na vitendo vya ukandamizwaji wa haki za binadamu matukio yanayodaiwa kufanyika nchini Libya. Uhalifu huo kwa kiasi kikubwa unadaiwa kufanywa na vikosi vitiifu kwa utawala wa Gaddafi licha kwamba ripoti nyingine zinavitaja vikosi vya waasi kuwa ni sehemu ya matukio hayo.

Hali ya wasiwasi pia imezidi kujitokeza kufuatia kutojulikana waliko wafungwa kadhaa ambao walitiwa gerezani wakati wa utawala wa Gaddafi kabla na baada ya machafuko kuanza. Kamishna ya haki za binadamu imevitaka vikosi vitiifu kwa Gaddafi kufichua kule waliko wafungwa hao kabla maisha yao hayajapotezwa.

Rupert Colville ni msemaji wa ofisi ya haki za binadamu