Zaidi ya watoto milioni moja wahitaji misaada ya dharura kusini mwa Somalia
Huku takriban watoto milioni 1.5 kote nchini Somalia wakiwa wanahitaji misaada ya kuokoa maisha na wengine 640,000 wakisumbuliwa na utapiamlo shirika la kuhudumia watoto la Umoja wa Mataifa UNICEF limetoa wito kwa washika dau wote kulipa kipau mbele suala la kuokoa maisha na kufanya jitihada za kuwafikia watoto wanaohitaji usaidizi.
Ili kuwafkia watoto hao kwa haraka UNICEF pamoja na washirika wake wameanzisha mikakati ya kuhakikisha kuwa misaada imefika kwenye maeneo waliko. Marixie Marcado ni msemaji wa UNICEF.
(SAUTI MARIXIE MARCADO)