Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

AMISOM yakabilina na makundi yanayozuia usambazaji wa misaada Somalia

AMISOM yakabilina na makundi yanayozuia usambazaji wa misaada Somalia

Huku shughuli za kutoa misaada kwa watu wanaokumbwa na njaa nchini Somalia zikiendelea bado makundi ya wanamgambo yanaendelea kutatiza shughuli huku wakiweka vizuizi barani na kuwazuia wale wanaoikimbia maeneo yanayokumwa na njaa.

Hata hivyo kikosi cha UM cha kulinda amani nchini Somalia AMISOM kinafanya kila kiwezalo kuhakiksha kuwa huduma hizo zinawafikia wanaozitaji. Haya ni kulinga na kamanda wa kikosi cha AMISOM Meja Jenerali Nathan Mugisha ambaye yuko mjini New York kuhudhuria mkutano wa makamanda vya vikosi vya Umoja wa Mataifa nilipozungumza naye kwenye studio za UM.