Ni wakati wa kubadili sera za makazi nchini Algeria: Rolnik
Mjumbe maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu haki ya kuwa na makao Raquel Rolnik ameipongeza Algeria kutokana na kujitolea kwake katika kuimarisha sekta ya makazi na kiasi kikubwa cha fedha kinachotengewa sekta hiyo.
Akikamilisha ziara iliyomchukua siku kumi nchini Algeria Rolnik hata hivyo amesema kuwa juhudi hizi ni muhimu katika kiwango cha kimataifa kinyume na nchi nyingi ambazo hazitilii maanani sekta ya makazi .
(SAUTI YA Maureen koech)