Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Nchi za pembe ya Afrika zaendelea kukumbwa na uhaba mkubwa wa chakula

Nchi za pembe ya Afrika zaendelea kukumbwa na uhaba mkubwa wa chakula

Ripoti zimekuwa zikitolewa kuhusu hali kwenye pembe ya Afrika baada ya eneo hilo kukumbwa na ukame wa muda mrefu. Kwa sasa kuna uhaba mkubwa wa chakula nchini Somalia , Ethiopia , Kenya na Uganda hali ambayo huenda ikawa janga kubwa zaidi dunia ikiwa hatua za dharura hazitachukuliwa kulingana na mkuu wa shirika la kuwahudumia wakimbizi la Umoja wa Mataifa UNHCR Antonio Gutteres . Msemaji wa UNHCR nchini Kenya Immanuuel Nyabera amezungumza na mwandishi wetu Jason Nyakundi na kumwelezea jinsi hali ilivyo.

(MAHOJIANO YA JASON NA IMMANUEL NYABERA )