Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UM waitaka China kuheshimu haki za binadamu

UM waitaka China kuheshimu haki za binadamu

Kundi la wataalamu wa Umoja wa Mataifa lenye shabaya ya kutekelezwa kwa maazimio kadhaa limeitolea mwito China kubainisha mahala inapowashikilia watu kadhaa ikiwemo wafuas wa mrengo wa Tibet walilokamatwa na kupelekwa sehemu isiyojulikana.

Mapema mwezi April mwaka huu, serikali ya China iliwakamata watu zaidi ya 300 wa mafungamano ya Ngaba Kirti na ya kupelekwa katika sehemu isiyojulikana hadi sasa. Tukio hilo linadaiwa kuendeshw ana vikosi vya polisi vikishirikiana na  Kikosi cha usalama  wa taifa na Jeshi la Ukombozi wa China.

Ikielezea tukio hilo, Umoja wa Mataifa umeitaka mamlaka China kutoa taari za

kweli juu ya tukio hilo na kueleza bayana mahala inapowashikilia watu hao.

Wataalamu hao wameionya China kuwa inawajibika kuheshimu na sheria za kimataifa

 juu ya haki za binadamu.