Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Japan ilikadiria kwa upungufu athari za tsunami kwenye mitambo yake ya nyukilia

Japan ilikadiria kwa upungufu athari za tsunami kwenye mitambo yake ya nyukilia

Uongozi wa Japan huenda ulikadiria kwa mapungufu athari za tsunami kwenye kinu chake cha nyuklia cha Fukushima Daiichi kwa mujibu wa shirika la kimataifa la nguvu za atomic IAEA.

Uharibifu mkubwa kwenye kinu hicho umeelezewa kuwa ndio mbaya zaidi tangu ajali ya nyuklia ya Chernobly. Uharibifu huo umetokea baada ya tsunami nchini Japan iliyosababishwa na tetemeko kubwa la ardhi. Hayo yameelezwa na ripoti ya wataalamu wa IAEA wa nyuklia waliozuru Japan kwenye mtambo huo hivi karibuni. George Njogopa anayo ripoti kamili.

(RIPOTI YA GEORGE NJOGOPA)