Shirika la kimataifa la uhamiaji linasaidia watu wanaokimbia machafuko Abyei
Mpango wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan umesema wakati maelfu ya watu wakikimbia jimbo la Abyei Sudan kutokana na machafuko na kuelekea Sudan Kusini, mashirika ya misaada yanaongeza juhudi za msaada wa kibinadamu.
Jumbe Omari Jumbe , msemaji wa Shirika la kimataifa la uhamiaji (IOM) amezungumza na Redio ya Umoja wa Mataifa hii leo juu ya hali katika eneo la Abyei na juhudi za IOM kuwasaidia wale wanaokimbia machafuko jimbo hilo la Sudan.