Michezo itumike kuharakisha maendeleo duniani:Ban
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon amezitolea mwito nchi zote ulimwenguni kuhakikisha kwamba zinaowanisha mipango yao na shughuli za kimichezo kwa ajili ya kusukuma mbele maendeleo.
Akizungumza mjini Geneva kwenye kongamano la pili linalojadilia masuala ya michezo, amani na maendeleo, Ban amesema kuwa nchi nyingi dunia zinapaswa kuchukua hatua hiyo kwani michezo inanafasi kubwa ya kuchangia kwenye ufikiaji wa shabaya ya malengo ya maendeleo ya mellenia.
Ameongeza kuwa Umoja wa Mataifa daima unadhamini na kutambua umuhimu wa michezo na ndiyo maana mara nyingi hutumia michezo ili kuzisaidia jamii nyingi duniani.