Tutu akabidhi uongozi wa kupambana na HIV
Askofu mkuu wa Afrika ya Kusini Desmond Tutu leo amekabidhi jukumu la kupambana na HIV na ukimwi kwa viongozi vijana wa kizazi kipya.
Makabidhiano hayo yamefanyika katika hafla maalumu iliyoandaliwa ili kuchagiza mabadiliko ya vita dhidi ya ukimwi Robben nchini Afrika Kusini.
Hafla hiyo iliyokutanisha viongozi wa ngazi za juu wa dunia kutoka tume za kupambana na ukimwi imeandaliwa kwa ushirikiano na shirika la Umoja wa mataifa la kupambana na ukimwi UNAIDS. Jason Nyakundi anaarifu.
(Ripoti ya Jason Nyakundi)