Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Ukuaji wa miji unashika kasi , ni lazima uende sambamba na miundombinu bora:UN-HABITAT

Ukuaji wa miji unashika kasi , ni lazima uende sambamba na miundombinu bora:UN-HABITAT

Shirika la Umoja wa Mataifa la makazi UN-HABITAT mwezi huu liliandaa mkutano wa kimataifa mjini Nairobi Kenya yaliko makao makuu ya shirika hilo na kuhudhuriwa na wakilishi kutoka nchi mbalimbali duniani.

 

Mada kuu ya mkutano huo maendeleo endelevu maeneo ya mijini kwa kupitia uwezaji wa kupata ardhi, nyumba, huduma muhimu na miundombinu.

Mawaziri wanaohusika na masuala ya miundombinu na makazi walipata fursa ya kueleza mipango waliyonayo katika nchi zao kuhusu ukuaji wa miji, kuhakikisha unakwenda bega kwa bega na upatikanaji wa huduma muhimu, kulinda mazingira, na maendeleo.

Mwandishi wetu mjini Nairobi Jason Nyakundi alikwenda kwenye mkutano huo na kupata fursa ya kuzungumza na baadhi ya watu waliohudhuria kutoka mataifa ya Afrika na kuandaa makala hii.

(MAKALA NA JASON NYAKUNDI)