Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

IOM yafungua zahanati mpaka wa Kenya na Uganda

IOM yafungua zahanati mpaka wa Kenya na Uganda

Shirika la kimataifa la uhamiaji IOM kwa ushirikiano na baraza la kupambana na Ukimwi nchini Kenya wamefungua zahanati mpya ya kutoa matibabu ya bure ili kuwafikia wasio na uwezo wa kugharamia matibabu na wanaosafiri kati ya mpaka wa Kenya na Uganda.

Zahanati hiyo iliyofunguliwa kwenye mji wa Busia katika mkoa wa Magharibi nchini Kenya itawahudumia wasafiri na kutoa matibabu ya bure dhidhi ya magonjwa kadha ukiwemo ugonjwa wa kifua kikuu , Malaria na Ukimwi. George Njogopa anaripoti

(RIPOTI YA GEORGE NJOGOPA)