Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mauaji ya mpiga picha wa kituo kimoja cha runinga nchini Libya kuchunguzwa :UNESCO

Mauaji ya mpiga picha wa kituo kimoja cha runinga nchini Libya kuchunguzwa :UNESCO

Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa lenye jukumu la kulinda uhuru wa waandishi wa habari ameshutumu mauaji ya mpiga picha wa kituo cha runinga cha Al Jazeera ambaye aliuawa baada ya kuvamiwa kwenye vitongi vya mji wa Benghazi ulio mashariki mwa Libya.

Ali Hassan Al- Jaber alikuwa akirejea kwenye mji huo unaoshikiliwa na waasi baada ya kuripoti hanari kwenye mji ulio karibu ambapo watu wasiojulikana waliokuwa wamejihami walilifyatulia risasi gari lake.