Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNCTAD yazindua kitabu cha uchumi unaojali mazingira

UNCTAD yazindua kitabu cha uchumi unaojali mazingira

Shirika la umoja wa mataifa linalohusika na maendeleo ya viwanda (UNCTAD), limechapisha kitabu chake katika mfululizo wa matoleo yake kinachoangazia uchumi unaojali mazingira.

Kikiwa na shabaya ya kuelezea umuhimu wa kuhimiza uchumi unaojali mazingira, kitabu hicho kimeelezea kwa kina ni vipi ulimwengu utakavyoweza kuzikwepa changamoto za mabadiliko ya tabia nchi kwa kutilia uzito uchumi wa mfumo huo.

 

Kitabu hicho kimezingatia maazimio yaliyofikiwa kwenye mkutano wa umoja wa mataifa wa mwaka 1992 uliofanyika huko Rio de Janeiro, kinatoa mwongozo utakaosaidia kuzishawishi nchi mbalimbali kutekeleza sera za uchumi endelevu ambao pia utazingatia pia mazingira.

 

Kuna sura kadhaa ndani ya kitabu hicho ambazo zimegawika kwa kuzingatia sera, mipango ya kiuchumi ambayo mataifa duniani yanashauriwa kutekeleza