Maafisa wa UM wawasili Burundi
Tume ya Umoja wa Mataifa ya kuimarisha amani nchini Burundi imeo ziarani
nchini humo kukadiria wapi umefikia mpango wa amani baada ya nchi hiyo
kupitia vipindi vingumu ikiwa ni pamoja na vita vya wenyewe kawa wenyewe.
Balozi wa Uswizi katika Umoja wa Mataifa Paul SEGER anayeongoza tume hiyo amesema hali ilioko nchini humo inaleta matumaini kwa taifa hilo kuelekea kustawi.
Licha ya tume hiyo kuhimiza kuwepo mazungumzo ya kuzihusisha pande zote baada ya uchaguzi mkuu ulioshuhudia CNDD/FDD wakishinda ,hata serikali imepinga hoja zozote za kugawana madaraka.
(SAUTI YA RAMADHANI KIBUGA)