Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Ukame waiweka Somalia kwenye wakati mbaya zaidi

Ukame waiweka Somalia kwenye wakati mbaya zaidi

Zaidi ya watu milioni 7 nchini Somalia wapo kwenye hali ngumu na majaliwa ya nchi hiyo bado ni tete hasa kutokana na kitisho cha kuzuka kwa hali ya ukame ambao unaiyakabili maeneo mengi ya nchi

Kwa mujibu wa hali ya tathmini iliyotolewa na mkuu wa shirika la umoja wa mataifa linalohusika na masuala ya usamaria mwema. Somalia kwa hivi sasa ipo katikati ya kitovu cha majanga ikiwemo kukosekana kwa utengamao wa kisiasa na majanga ya kimaumbile.

 

Bi Valerie Amos ambaye hivi karibuni amelitembelea eneo hilo amesema kuwa hali ya ukame imeanza kujitokeza kwenye maeneo yanayomilikiwa na makundi ya waasi.

(SAUTI YA VALERIE AMOS)