Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Bei ya chakula yaendelea kupanda duniani-Benki ya Dunia

Bei ya chakula yaendelea kupanda duniani-Benki ya Dunia

Ripoti moja iliyotolewa na Benki ya Dunia inaonyesha kuwepo kwa ongezeko kubwa

la bei ya chakula kwa nchi zinazoendelea, hatua ambayo inazusha hali ya wasiwasi

kwa mamilioni ya watu ambao hali zao ni za kipato cha chini.

Ongezeko hilo la bei lililoanza tangu june mwaka jana na kuendelea kupanda hadi sasa limesababisha zaidi ya  watu  milioni 44 kuangukia kwenye umaskini.

 

Kwa mujibu wa ripoti hiyo iliyotolewa wakati maafisa wa ngazi za juu wa benki hiyo wakijiandaa kwa mkutano mhimu huko Paris, ongezeko hilo la kiwango 15 asilimia limeanza kukaribia kile kiwango ilichojitokeza  mwaka 2008 wakati dunia ilipokumbwa na mtikisiko wa uchumi.

 

Viongozi wa benki hiyo ya dunia wanaokutana huo Paris  wanatazamia kutilia uzito

ongezeko hilo la bei