Taasisi za kimataifa zimeshindwa kuwalinda waandishi wa habari:CPJ
Taasisi za kimataifa ambazo zinawajibika kulinda uhuru wa vyombo vya habari
zimelaumiwa kwa kushindwa kutekeleza wajibu wake huku ulimwengu ukishuhudia
waandishi wa habari wakiendelea kukabiliwa na hali za vitisho, kuwekwa
magerezani na wengine kuuwawa.
Taarifa iliyotolewa na kamati ya kulinda waandishi wa habari CPJ imesema kuwa waandishi wa habari duniani kote wameendelea kushuhudia mazingira magumu ya ufanyaji kazi na huku wengine wakipoteza maisha kutokana na uzembe wa mamlaka zinazohusika kushindwa kuwajibika.
Mkurugenzi wa mtendaji wa kamati hiyo Bwana Joel Simon amesema kuwa wakati sheria za kimataifa zinatambua uhalali wa kuwepo uhuru wa kujieleza lakini katika hali ya kushangaza matunda ya sheria hiyo inawaweka kando waandishi wa habari ambao mara zote wanakabiliwa na hali ngumu.
Kamati hiyo imeutaja Umoja wa Afrika kuwa ni miongoni mwa taasisi za kimataifa
ambazo zimeshindwa kusimamia vyema ulinzi wa waandishi wa habari
==