Wakimbizi wa Ivory Coast nchini Liberia wafikia 36,318
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR kwa kushirikiana na
kamishna ya kuwarejesha wakimbizi na kuwapa makazi ya Liberia, imewaandikisha
wakimbizi 36,318 ambao wameingia nchini humo kutoka Ivory Coast hadi kufikia
February 7 mwaka huu.
Idadi kubwa ya wakimbizi hao walioandikishwa ni watoto na wanawake ambao wanachukua kiasi cha asilimia 85. Wengi wa wakimbizi hao ambao walianza kuwasili nchini humo tangu disemba mwaka jana, wanapatiwa hifadhi kwa jamii iliyopo mpakani mwa Liberia na Ivory Coast.
Marixie Mercado ni msemaji wa UNICEF:
(SAUTI YA MARIXIE MERCADO)