Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNHCR na tume ya ulaya wanazuru Yemen kutathmini hali ya wakimbizi wa ndani

UNHCR na tume ya ulaya wanazuru Yemen kutathmini hali ya wakimbizi wa ndani

Kamishina mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR bwana Antonio Guterres na kamishina wa tume ya muungano wa Ulaya ya ushirikiano wa kimataifa, msaada wa kibinadamu na kukabili majanga Kristalina Georgieva wamewsili Yemen leo katika ziara yao ya kwanza ya kikazi pamoja.

Katika ziara hiyo ya siku tatu itakayokamilika Januari 15 watatathimini operesheni za msaada kwa wakimbizi wa ndani Kaskazini mwa nchi hiyo na changamoto zinazotokana na ongezeko la wakimbizi wa Kisomali wanaovuka Gghuba ya Aden na bahari ya Sham na kuingia nchini humo. George Njogopa anaarifu.

(SAUTI YA GEORGE NJOGOPA)