Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Wakimbizi waanza kutembelewa na familia zao Sahara Magharibi:UM

Wakimbizi waanza kutembelewa na familia zao Sahara Magharibi:UM

Wakimbizi wa Sahrawi kutoka Sahara Magharibi ambao walitengana na familia zao kwa zaidi ya miaka 30 wameanza kutembelewa leo.

Familia za wakimbizi hao zimesafirishwa kwa ndege kutoka Sahara Magharibi hadi kambini nchini Aljeria. Wakimbizi wa Sahrawi walianza kuwasili Aljeria mwaka 1976 baada ya Hispania kuondoka Sahara Magharibi na kuzuka machafuko. Shughuli za kuwakutanisha wakimbizi na familia zao zinafanywa na shirika la Umoja wa Mataifa la wakimbizi UNHCR. George Njogopa anaripoti.

(SAUTI YA GEORGE NJOGOPA)