Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

WFP yajiandaa kukabili njaa baada ya kura ya maoni Sudan

WFP yajiandaa kukabili njaa baada ya kura ya maoni Sudan

Wakati Sudan Kusini inajiandaa kupiga kura ya maoni mwishoni mwa wiki hii, shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula WFP linajitahidi kuhakikisha kura hiyo ya kihistoria haita changia njaa zaidi katika eneo hilo ambalo limeghubikwa na miongo ya vita na majanga ya asili.

WFP inasema ni wakati muhimu sana na njia panda ya kisiasa Sudan nchi ambayo imeghubikwa na miongo ya vita na njaa, na imeweka mikakati mine kukabili tatizo la njaa likizuka. Jason Nyakundi na taarifa kamili.

(SAUTI YA JASON NYAKUNDI)