Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Watu walioathirika na mafuriko Pakistan bado wanahitaji msaada: UM

Watu walioathirika na mafuriko Pakistan bado wanahitaji msaada: UM

Taarifa ya pamoja iliyotolewa na mwakilishi maalumu wa Umoja wa Mataifa nchini Pakistan balozi Rauf Engin Soysal na mratibu wa Umoja wa Mataifa nchini Pakistan Tomo Pakkala inasema mamilioni ya wapakistan bado wanahitaji msaada kukabili athari za mafuriko yaliyowakumba.

Mafuriko hayo ya yalisababisha mtafaruku mkubwa wa kibinadamu kuwahi kuikumba Pakistan na kuathiri watu takribani milioni 20. Maafisa hao wamesema kwa nia walionayo watu wa Pakistan, kwa msaada wa kitaifa na Kimataifa nchi hiyo itazishinda changamoto za mafuriko hayo.

Wameongeza kuwa Umoja wa Mataifa utaendelea kuwasaidia watu wa Pakistan watakapohitaji msaada kupitia miradi na mipango yake mbalimbali.