Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Ulaya yatakiwa kuongoza misaada kwa nchi maskini:BAN

Ulaya yatakiwa kuongoza misaada kwa nchi maskini:BAN

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon amesema kuwa muungano wa ulaya unaweza kuongoza kuwepo kwa ushirikiano wa kimaendeleo katika kusaidia nchi maskini.

Juma lililiopita Ban alitoa wito wa kuwepo kwa ushirikiano katika masuala kadha yakiwemo ya usalama kati ya Umoja wa Mataifa na shirika la usalama barani ulaya lililo na wanachama 56 kutoka Marekani kwenda ulaya na kati kati mwa bara Asia.