Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Njia ya kuafikia makubaliano ya Cancun yaanza kujitokeza-UM

Njia ya kuafikia makubaliano ya Cancun yaanza kujitokeza-UM

Mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu mabadiliko ya hali ya hewa unaondelea mijini Cancun Mexico unaingia wiki yake ya pili ambapo pia ni mkutano wa sita wa nchi wanachama kwenye makubaliano ya Kyoto .

Vyombo vya Umoja wa Mataifa vinavyoshughulikia mpango wa uratibuji mazingira vinamatumaini kwamba mkutano wa Cancún, Mexico ambao unajadilia changamoto za mazingira huenda ukafikia makubaliano. Kati ya wanaohudhuria mkutano huu ni bibi Rahima Njaidi mkurugenzi wa shirika la Mjumita nchini Tanzania na alizungumza na Jerome Longue wa Redio ya Umoja wa Mataifa:

(SAUTI YA RAHIMA NJAIDI)