Siku ya kimataifa ya kupinga ukatili dhidi ya wanawake
Kila mwaka tarehe 25 Novemba ni siku ya kimataifa ya kupinga ukatili dhidi ya wanawake na wito umetolewa kwa serikali, jumuiya za kijamii, mashirika yasiyo ya kiserikali na wadau wote wanaopigania haki za wanawake kuhakikisha udhalimu huo unamalizwa.
Kikubwa nchi zimesisitizwa kuweka sheria kali dhidi ya wadhalimu iwe ni katika unyanyasaji wa majumbani, ubakaji, kunyimwa haki za binadamu na mila na desturi zingine zinazomrudisha nyuma mwanamke. Flora Nducha ameandaa makala hii maalumu kuhusu siku ya leo, ungana naye.