Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Maelfu ya wapakistan kuadhimisha Eid al-Adha

Maelfu ya wapakistan kuadhimisha Eid al-Adha

Hata baada ya mafuriko makubwa kuikumba Pakistan mapema mwezi huu maelfu ya watu kwenye mkoa wa Punjap wataungana na waislamu wengine duniani kusherehekea Eid al-Aidha juma hili.

Waliolazimishwa kuhama makwao wanasema kuwa watamtoa mbuzi kafara na kuandaa chakula kwa watu wa familia zao. Maelfu ya wenyeji wengine wa Punjap waliopoteza makao , mali na mifugo pia watakuwa wakisherehekea. Huyu tena George Njogopa:

Waumini wa dini ya kiislamu duniani kote wameadhimisha siku kuu ya Idd al Hajji ambayo imeangukia siku ya jumatano. Siku hiyo inaadhimishwa kama ishara ya kumbukumbu wakati Ibrahim alipojaribiwa na shetani asimchinje mwanae kwa ajili ya sadaka takatifu wa Mungu. Waumini wengi wa dini hii wameadhimisha siku hiyo kwa kuchinja ng'ombe, mbuzi, kondoaa na ngamia.

Nchini Pakistani katika jimbo la Punjab ambalo hivi karibuni lilikubwa na mafuriko makubwa na kuharibu kabisa ekari za mashamba, wananchi