Mkutano wa nne juu ya mkataba wa matumizi ya tumbaku kufanyika Uruguay
Mkutano wa nne wa kimataifa unaojadiliwa juu ya mkataba wa matumizi ya tumbaku unatazamiwa kufanyika huko: Punta del Este, Uruguay kuanzia Novemba 15-20.
Wajumbe zaidi ya 600 kutoka nchi zaidi ya 170 wanatazamiwa kuhudhuria mkutano huo na wanatazamiwa kuibua mikakati mipya itayofanikisha utekelezaji wa mkataba huo.