Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNHCR yatoa wito kuwalinda wakimbizi wa Kisomali kenya

UNHCR yatoa wito kuwalinda wakimbizi wa Kisomali kenya

Shirika la kuwahudumia wakimbizi la Umoja wa Mataifa UNHCR limeelezea kusikitishwa kwake kuhusu hatima ya zaidi ya wakimbizi 8000 kutoka Somali walioamrishwa kuondoka eneo la Mandera lililo kaskazini mashariki mwa Kenya mnamo juma hili.

Hata hivyo wengi wa wakimbizi hao walielekea katika eneo lisilomilikiwa naa nchi yoyote kati ya mpaka wa Kenya na Somali na kukataa kuendelea mbele kwenda Somali. George Njogopa na taarifa kamili.

(RIPOTI YA GEORGE NJOGOPA)