Waathiriwa wa mafuriko Pakistan huenda wakakabiliwa na njaa:IFRC
Shirikisho la kimataifa la chama cha msalaba mwekundu IFCR limetoa wito kwa jamii ya kimataifa kujitokeza kuhakikisha kuwa mamilioni ya waathiriwa wa mafuriko hawaishi njaa wakati majira wa baridi.
Wito huu umetolewa kwenye mkutano wa chama cha msalaba mwekundu cha Pakistan uliondaliwa mjini Doha ambapo waakilishi kutoka mashirika 20 ya vyama vya msalaba mwekundu kutoka sehemu mbali mbali duniani wamekusanyika kujadili mipangoya kusaidia chama cha msalaba mwekundu cha Pakistan kutoa huduma kwa watu milioni mbili waliothirika na mafuriko kwa muda wa miaka miwili iyajo. George Njogopa na Taarifa zaidi
(RIPOTI YA GEORGE NJOGOPA)