Ripoti ya UM kuhusu ukiukaji wa haki za binadamu DR Congo yaishutumu Rwanda na Uganda
Ripoti ya Umoja wa Mataifa iliyoandaliwa na ofisi ya tume ya haki za binadamu imetoka leo ikielezea ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu uliofanyika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kati ya mwaka 1993 na 2003.
Akizungumza na Radio ya Umoja wa Mataifa mkuu wa haki za binadamu Navi Pillay amesema ripoti hiyo ni ya kukabiliana na ukwepaji wa sheria na kuhakikisha wahusika wanafikishwa kunakostahili kwani mamilioni ya watu wameathirika na uasi huo.
(SAUTI NAVI PILLAY)
(SAUTI RUHAKANA RUGUNDA)
Na kuhusu tishio la awali la Uganda kwanba ripoti hiyo ikiyoka itaathiri ushiriki wa mipango ya amani ya kikanda Rugunda amesema
(SAUTI RUHAKANA RUGUNDA)
Nchi nyingine zilizoguswa katika ripoti hiyo ni Burundi, Zimbabwe na Angola. Na waziri wa mambo ya nje ya Angola Georges Chikoti amesema ripoti hiyo haikuzingatia taratibu zinazotakiwa.
(SAUTI GEORGES CHIKOTI)