Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Leo inasherehekewa siku ya kimataifa ya utalii

Leo inasherehekewa siku ya kimataifa ya utalii

Leo ni siku ya kimataifa ya utalii, ambayo mwaka huu inaadhimishwa kwa kauli mbiu utalii na bayo-anuai.

Katika ujumbe maalumu wa kuadhimisha siku hii Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon amesema utalii na masuala ya bayo-anuai vinakwenda sambamba na haviwezi kutenganishwa. Amesema mwaka huu ambao ni mwaka wa bayo-anuai unatoa fursa muafaka ya kujikita katika juhudi za haraka za kulinda bayo-anuai kwa ajili ya utajiri, afya na maslahi ya watu katika nchi zote duniani.

Ban pia ameipongeza sekta ya utalii duniani kwa kutambua umuhuimu wa kulinda bayo-anuai na ametoa wito kwa pande zote kuimarisha jukumu lao la kuendeleza ulinzi huo.