Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Viongozi wa Afrika wataka mabadiliko kwenye UM:Kagame

Viongozi wa Afrika wataka mabadiliko kwenye UM:Kagame

Viongozi mbalimbali kutoka barani Afrika wametoa wito wa kufanyiwa marekebisho Umoja wa Mataifa na baraza la usalama.

Viongozi hao wamesema imefika wakati wa Afrika kupata nafasi ya kudumu kwenye baraza la usalama na pia kupewa nafasi ya kusikilizwa zaidi kama wengine kutoka mataifa yaliyoendelea.

Rais Paul Kagame wa Rwanda akihutubia mjada huo amesema hakuna usawa wa mawazo miongoni wa wajumbe wa Umoja wa Mataifa.

(SAUTI PAUL KAGAME)