Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UM umelaani walowezi wa Israel kuvamia nyumba za Wapalestina

UM umelaani walowezi wa Israel kuvamia nyumba za Wapalestina

Mratibu maalumu wa Umoja wa Mataifa kwa ajili ya mchakato wa amani ya Mashariki ya Kati ,leo amelaani hatua ya walowezi wa Israel wenye silaha kuvamia kwa nguvu jengo kwenye mji wa zamani wa Jerusalem.

Mratibu maalumu wa Umoja wa Mataifa kwa ajili ya mchakato wa amani ya Mashariki ya Kati ,leo amelaani hatua ya walowezi wa Israel wenye silaha kuvamia kwa nguvu jengo kwenye mji wa zamani wa Jerusalem . Mji huo una una nyumba za familia tisa za Wapalestina na ametoa wito kwa serikali kuchukua hatua mara moja.

Katika taarifa yake mratibu huyo Robert Serry amesema kitendo hicho hakikubaliki na naitolea wito serikali kuwaondoa walowezi hao kutoka kwenye nyumba ya Wapalestina na kurejesha mambo kama yalivyokuwa.

Tafrani hiyo inafuatia hatua ya jana ya serikali ya Israel kubomoa majengo kadhaa ya biashara ya Wapalestina nje kidogo ya mji wa Jerusalem Mashariki.