Wapinzani nchini Burundi wapinga ziara ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa
Wapinzani nchini Burundi wamekemea vikali ziara ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon itakayoanza kesho Jumatano.
Mwakilishi wa Umoja wa Mataifa nchini Burundi Charles Petrie amewataka wapinzani hao kuwasilisha kero zao. Mwandishi wetu wa Bujumbura Ramadhan Kibuga ametutumia taarifa hii.