Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mwalishi wa UM nchini Afghanistan alaani mashambulizi dhidi ya majengo ya serikali

Mwalishi wa UM nchini Afghanistan alaani mashambulizi dhidi ya majengo ya serikali

Mwakilishi maalumu wa Umoja wa Matafa nchini Afghanistan Staffan de Mistura leo amelaani mashambulizi dhidi ya majengo ya serikali katika eneo la Kusini Magharibi mwa nchi hiyo ambayo ametaja kama ya kusikitisha.

Duru zinasema , Gul Makai Wakil, mwanacham wa serikali ya kimkoa pamoja na maafisa watatu waliuwawa katika shambulizi hilo ambalo lilijibizwa na wanajeshi na polisi wa Afghanistan katika eneo la Zaranj, mjii mkuu wa mkoa wa Nimroz. Raia wanne na maafisa saba walijeruhiwa katika tukio hilo.

Bi Gul Makai ambaye ni mtunzi wa mashairi , amekuwa msitari wa mbele kupigania haki za akina mama mjini Zaranj, anaheshimiwa na wakaazi wa eneo lake kwa kuwa na mtazamo wa kitaifa kwa Afghanistan.