Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Muongozo mpya kuhusu dawa za watoto watolewa na WHO na UNICEF

Muongozo mpya kuhusu dawa za watoto watolewa na WHO na UNICEF

Mashirika mawaili ya Umoja wa Mataifa yametoa muongozo mpya kwenye wavuti wa wapi unaweza kupata dawa zilizotengenezwa kwa ajili ya watoto.

Muongozo huo ulioandaliwa na shirika la afya duniani WHO na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF, unaweza kuzuia vifo vya watoto milioni tisa kila mwaka vitokanavyo na maradhi ambayo ynaweza kuzuilika na kutibika.

Mkurugenzi wa madawa na sera wa WHO Hans Hogerzeil amesema kuimarisha upatikanaji na uwezo wa kupata dawa za watoto bado ni tatizo kubwa kwa watoto wengi walioko kwenye nchi masikini.

Muongozo huo ambao pia unaelezea wapi pa kupata dawa na bei zake kwa baadhi ya dawa utawasaidia madaktari na mashirika kupata dawa muhimu aina 240 ambazo zitaokoa maisha ya watoto.