Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mratibu wa UM wa masuala ya kibinadamu amezuru Kivu DRC

Mratibu wa UM wa masuala ya kibinadamu amezuru Kivu DRC

Mratibu wa Umoja wa Mataifa wa masuala ya kibinadamu na misaada ya dharura John Holmes ambaye yuko ziarani Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo , leo amezuru jimbo la Kivu ya Kusini.

Akiwa Kivu ametembelea kambi ya wakimbizi wa ndani iliyoko Mwenga takribani kilometa 80 kusini magharibi mwa mji wa Bukavu na kukutana na viongozi wa eneo hilo na wafanyakazi wa misaada.

Katika mkutano wao amesisitiza kuwalinda raia, kusambaza misaada ya kibinadamu na kuahakikisha misaada hiyo inawafikia walenga ni jukumu la serikali .Kivu Kusini ni kitovu cha mapambano baiana ya jeshi la serikali na wanamgambo wa Kihutu kutoka Rwanda wa FDLR. Kivu hivi sasa kuna wakimbizi wa ndani milioni 1.4.