Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

WHO imewataka wazazi Uchina kuwapeleka watoto kupata chanjo ya Surua na Hepatitis B

WHO imewataka wazazi Uchina kuwapeleka watoto kupata chanjo ya Surua na Hepatitis B

Shirika la afya duniani WHO leo limewataka wazazi nchini Uchina kuwalinda watoto wao dhidi ya vifo vya mapema na matatizo ya muda mrefu ya maini kwa kuwapa chanjo ya surua na homa ya manjano au hepatitis B.

Uamuzi wa chanjo Uchina umefanyika kwa majadiliano na WHO kwa kuzingatia mafanikio ya nchi zingine zilizofanya kampeni ya kitaifa ya chanjo hiyo.