Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Katibu Mkuu wa UM yuko Vienna ambako amekutana na viongozi wa nchi hiyo

Katibu Mkuu wa UM yuko Vienna ambako amekutana na viongozi wa nchi hiyo

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa yuko Vienna Austria ambako amefanya mazungumzo na waziri wa mambo ya nje anayehusika na masuala ya Ulaya na uhusiano wa kimataifa Michael Spindelegger.

Bwana Ban Ki-moon amesema mkutano wao umekuwa wa mafanikio na wamejadili masuala mbalimbali ikiwemo juhudi za kuleta amani na usalama. Katika suala hilo wamezungumzia ushiriki wa vikosi vya kulinda amani vya Austria na Ban amewapongeza askari wa kike na wakiume wanaoshiriki operesheni hizo.

Ban amemuomba waziri huyo wa mambo ya nje wa Austria kuishawishi serikali kuongeza idadi ya wanawake polisi katika shughuli za kulinda amani na kusuluhisha migogoro. Mbali ya hayo wamejadili haja ya Austria kuunga mkono juhudi za amani mashariki ya kati na hatua ya Marekani na Urusi kutaka kupunguza silaha za nyuklia