Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

El-nino bado inaendelea kuathiri sehemu mbalimbali duniani

El-nino bado inaendelea kuathiri sehemu mbalimbali duniani

Shirika la kimataifa la utabiri wa hali ya hewa WMO limesema matukio ya Elnino yanaendelea kusambaa na kuwa na athari kubwa.

Athari hizo za El Nino zilizoanza Juni 2009 sasa zinaonekana katika bahari ya Pasific na katika mabadiliko ya hali ya hewa katika sehemu nyingi duniani.

Na inatabiriwa kuwa athari kubwa zaidi za El Nino zitajitokeza katikatoi ya mwaka huu wa 2010 katika mwambao wa Pasific.Hatahivyo imebainika kuwa mwezi Machi hadi Juni huwa ni mgumu katika utabiri, kama anavyofafanua msemaji wa WMO.