Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mapigano Somalia yazidi kuwaathiri raia

Mapigano Somalia yazidi kuwaathiri raia

Mapigano baina ya majeshi ya serikali na wanamgambo wa Al-Shabaab nchini mjini Moghadishu Somalia yanazidi kuwafungisha virago maelfu ya raia.

Inaarifiwa kwamba raia 24 wameuawa katika mapigano yaliyozuka siku ya jumatano. Baadhi ya raia wameanza kuukimbia mji wa Moghadishu mapema kufuatia taarifa majeshi ya serikali yanajiandaa kufanya mashambulizi makubwa dhidi ya wanamgambo hao. Melisa Fleming msemaji wa UNHCR anafafanua kuhusu hali halisi