UNHCR: Operesheni za kijeshi na uhalifu zinasababisha wimbi jipya la wakimbizi
Idara inayowahudumia Wakimbizi ya UM, UNHCR inasema kuendelea kwa operesheni za kijeshi dhidi ya wapiganaji wa kihutu na makundi ya wahalifu wenye silaha katika jimbo linalokumbwa na ghasia la Kivu ya Kaskazini huko DRC kumesababisha maelfu ya watu kukimbia makazi yao mnamo miezi miwili ilyiopita.