Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Hali Chad Mashariki yazidi kuharibika, kuhadharisha OCHA

Hali Chad Mashariki yazidi kuharibika, kuhadharisha OCHA

Ofisi ya UM juu ya Misaada ya Dharura (OCHA) imeripoti hali ya usalama katika Chad Mashariki inaendelea kuwa mbaya zaidi. Mnamo mwisho wa wiki iliopita, msafara wa UM wa magari matatu ya kiraia, wa Shirika la UM juu ya Ulinzi Amani katika Jamuri ya Afrika ya Kati na Chad (MINURCAT) uliohusika na ugawaji wa misaada ya kihali kwa umma waathirika wa mapigano, ulishambuliwa na majambazi wasiojulikana wanane. Ofisa mmoja wa Vikosi vya Ulinzi wa Mchanganyiko, aliyekuwa akiongoza msafara wa UM, alijeruhiwa.