Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Wahamiaji wa JKK wakithiri katika taifa jirani kutafuta hifadhi baada kuzuka mapigano ya kikabila

Wahamiaji wa JKK wakithiri katika taifa jirani kutafuta hifadhi baada kuzuka mapigano ya kikabila

Shirika la UM Juu ya Huduma za Wahamiaji (UNHCR) limeripoti idadi ya raia wanaohajiri kutoka jimbo la Equateur, la kaskazini-magharibi katika JKK, inaendelea kuzidi kwa sababu ya kufumka kwa mapigano ya kikabila kwenye eneo lao.