Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNHCR inasema nusu ya wahamiaji duniani huishi mijini

UNHCR inasema nusu ya wahamiaji duniani huishi mijini

Shirika la UM juu ya Huduma za Wahamiaji (UNHCR) limeripoti kwamba zaidi ya asilimia 50 ya wahamiaji milioni 10.5 wanaosaidiwa na taasisi hii ya kimataifa, huwa wanaishi kwenye maeneo ya miji na miji mikuu ya sehemu mbalimbali za dunia.