Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Uspeni imeongeza maradufu mchango wake kwa WFP kupambana na njaa katika Pembe ya Afrika

Uspeni imeongeza maradufu mchango wake kwa WFP kupambana na njaa katika Pembe ya Afrika

Soraya Rodriguez Ramos, Waziri wa Nchi wa Uspeni kwa Ushirikiano wa Kimataifa, ametangaza siku ya leo kuwa serikali yao imekabidhi Shirika la UM juu ya Miradi ya Chakula Duniani (WFP) msaada wa Yuro milioni 75 (dola milioni 112) kutumiwa kufarajia hali mbaya ya chakula iliolivaa eneo la Pembe ya Afrika.